Saturday, May 26, 2012

DARASA MARIDHAWA KUTOKA KWA PROF.SHIVJI

Written by Ado Shaibu at udsm
 Issa Gulamhusein Shivji, yule msomi galacha katika medani ya sheria na utawala ameorodhesha (kupitia mihadhara yake ya ITV) yale aliyoyaita mapungufu makubwa ya utungaji wetu wa katiba tangu katiba ya uhuru 1961 mpaka katiba ya muungano ya mwaka 1977 inayotumika sasa.kwa mujibu wa prof.huyo wa kigoda cha mwalimu Nyerere katika umajumuhi wa Africa,upungufu mkubwa katika utungaji wa katiba zilizopita ni kama ifuatavyo;
1.kwamba katika uandikaji wa katiba zote,wananchi hawakushirikishwa ipasavyo.kwa mfano,katika uandikaji wa katiba ya mwaka 1977,wananchi hawakushirikishwa ipasavyo kutoa maoni yao.Hata wana CCM hawakushiriki kwa sababu chombo kikuu cha chama hicho,yaani mkutano mkuu,hakikuhusika.Iliyohusika ni halimashauri kuu.Jadi ya CCM ni kuyafanya yale yanayozungumzwa humo kuwa siri.
2.kwamba kutokana na kutoshirikisha wanachi ipasavyo,katiba zote zimekosa uhalali wa kisiasa(political legitmacy).lakini prof.shivji anataadharisha kwamba hii haimaanishi kwamba utawala wa mwalimu nyerere ulikosa uhalali wa kisiasa.uhalali ulikuwepo,bali haukutokana na katiba.ulitokana na itikadi ya CCM pamoja na umahiri na umaarufu wa mwalimu mwenyewe!
3.kwamba hata uhalali wa kisheria(legal legitimacy) una walakini!.kwa mujibu wa pro.shivji,historia ya utungaji wa katiba imejaa upuuzwaji na upindishaji wa hapa na pale wa matakwa ya kisheria.
4.kwamba hakukuwa na mjadala wa kitai katika utungaji wa katiba zote.Angalau,mjadala wa kitaifa ulikuwepo katika mabadiliko ya katiba ya mwaka1984 ambapo haki za binadamu ziliingizwa kwenye katiba.
Fikra hizi za prof.shivji pia zimefanyiwa tafakuri ya kina katika kitabu chake kipya kiitwacho INSHA ZA MAPAMBANO YA WANYONGE (hasa kwenye mada iitwayo "Madai ya katiba mpya:Unyonge wa katiba au Katiba ya wanyonge?''

TUKUMBUKE SAFARI YA MWISHO KATIKA MAISHA YETU

ALLAHU AKBAR !!




►You Are Rich ?
►You Are Strong ?
►You Are Independent ?
►You Don't Need Anyone ?

Okay Now, What About When You Die ???

►You NEED Someone To Clean Your Body,
►You NEED Someone To Cover Your Body With Kafan,
►You NEED Someone To Burry Your Body,
And . . . !!
The Most Important Thing, You NEED Some To Pray For You...
So, Don't Be ARROGANT...!! Be HUMBLE In This World...!!
Remember Shaitaan Was Not A Stupid But,
He Was ARROGANT...!!
[ A Very Good Reminder For Myself First ]
Only ALLAH Subhanahu Wata'ala Is The GREATEST,
The ONE,
The SUPREME,
And INDEPENDENT Of Anything/ Anybody . . .
ALLAHU AKBAR !!

Friday, May 25, 2012

SHUKRANI KWA WAISLAM WOTE KUTOKA KWA SHEKHE JUMA MKABAKULI KWAKUFANIKISHA HARUSI YAKE

Salaam za shukrani kutoka kwa ndugu  JUMA kwa wanafunzi wakitanzania waliosoma na wanaosoma nchini Algeria katika support yao ya kufanikisha Harusi yake,,, 
JUMA AHMED MKABAKULI ana haya yakusema
"Habari zenu wa ungwana, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wana-ATSA (ASSOCIATION OF TANZANIA STUDENTS IN ALGERIA) wote mlioudhuria kwenye harusi yangu na kwa msiofika kwa dua zenu njema.asanteni sana. Nilipata faraja ya hali ya juu sana nilipokuwa nanyi kwenye harusi yangu,
Kiukweli nimeyaona matunda ya undugu wa kweli wa wana-ATSA.
Mungu awazidishie kila la kheri katika maisha yenu.
Amen!"

Shekhe  JUMA AHMED MKABAKULI na mkewe katika harusi yao
Wadau waliomalinza elimu yao nchini Algeria na maswahiba wa kubwa wa Juma wakijaribu kushauri jambo katika sherehe za harusi ya Juma Mkabakuli ilioyo fanyika May 2012 jijini Dar es salaam
Timu ya wanafunzi waliosoma nchini Algeria wakiwa katika mlo wa pamoja katika harusi ya mwenzao jijini Dar es salam
Picha ya poamoja ya wadau (wanafunzi walio maliza nchin Algeria)  walioshirikiana bega kwa bega na Bw Juma Mkabakuli kufanikisha shughuli muhimu na njema.
"Blog na kwa miaba ya watanzania wote wasomao nchini Algeria tunawatakia kila la kheri wana ndoa hawa katika safari mpya ya maisha. ALL THE BEST JUMA and YOUR WIFE"

Manabii Wa Siku Za Mwisho

Manabii hawa walitabiriwa kwenye vitabu vingi vya dini, na sasa wapo na tunaishi nao tuji taadharishe naokwani nichachu ya kupotosha nafsi zetu,,,

Je mtu huyu analipwa na nani au anakula nini au anaishije yeye,,,?

Mbezi, leo asubuhi.

" Mwenyekiti, Waislamu Tumezidi Kulalamika!"


Ina lilah waina ilaihi rajoon. AN-NUUR (Mwangaza)!!!!!!!!!, kweli KUN FAY KUN. Hivi muhariri wa gazeti hili ana elimu gani?. Mbona tupo waislamu wengi tu tulifanya vizuri na mpaka leo hii tuna elimu za juu kabisa.

Waislam tumezidi kulalamika sana, Wallah adui mkubwa wa waislam ni sisi wenyewe waislam. Binafsi nilipomaliza degree yangu ya kwanza na kuomba kufundisha katika shule fulani ya kiislam, nilipewa offer ya mshahara wa alfu hamsini kwa mwezi na kuambiwa kuwa nifanye for 'sabbillah'-kwa ajili ya mwenyezimungu, ukweli nilifundisha mwezi mmoja siku ya mshahara sheikh akaniita ni kupatia alfu 20, na kusema nivute subira ntalipwa zilizobakia baadae. Kilichonifanya niache kazi na kwenda klufundisha shule ya mission kwa mshahara wa laki tano ni pale nilipoona mkuu wa chuo na walezi wakigawana kila ada inapolipwa na kufanya shule kama kijiwe cha kusubiri ada na kugawana kila siku.

Kinachoua shule za kiislam ni mismanagement. Shule hizi zinaendeshwa kimfumo wa madrass za kizamani zaidi ya shule za kisasa. Na mbaya zaidi unakuta mkuu wa shule ana elimu ya dini tu elimu dunia zero unatarajia nini hapo?

Hivi kama hufundishi wanafunzi, huna walimu bora unatarajia Jibrir awashukie wanafunzi wakati wa mtihani na kuwaambia 'Ikraa bismirabika raadhi halak'? na wao kujibu maswali yote ipasavyo?, lah! hiyo ilikuwa kwa mkumbe wa mwenyezi mungu tu Mtume Muhhamad (SAW). Bila maandalizi bora kwa wanafunzi hawawezi kufaulu.

Tuache kushabikia ujinga maana hata ukimpatia mtoto asiyejua kusoma dision one kwa ajili ya kuwafurahisha akina Sheikh Majaka wa An-nuur bado huko juu hatafika popote.

Heading kama hizi za An-nuur ndizo zinazidi kudidimiza elimu miongoni mwa waislam. Watoto wanaacha kusoma kwa bidii wakidhania kuwa majina yao ndiyo yatawafanya wafeli wakati mitihani inaandikwa namba mpaka stage ya mwisho kabisa baada ya kusahihishwa ndiyo majina yanawekwa kwa ajili ya kudisplay matokeo. Mimi nilifaulu la saba, nikaenda shule ya sekondari maalum ya serikali, nikafaulu form four kwa daraja la kwanza, nikafaulu form six kwa taraja la kwanza, nikafaulu, chuo kwa taraja la pili la juu, nikafaulu masters kwa daraja la kipekee (distinction), nimemaliza PhD kwa minor corrections, na majina yangu yote matatu ni 100% ya kiislamu.

Hii stori ya An0nuur imenikwaza sana Wallah, waandishi kama hawa ndiyo wanaudhalilisha uislam bila kijiju.

Mjumbe.

Thursday, May 24, 2012

MSAADAAA,,,,HEBU SOMA HII NDUGU YANGU KATIKA IMAN.

Nimeolewa Huku Nina Mimba Nini Hukumu Ya Mtoto Wa Kitendo Cha Zinaa?
SWALI:
Asalaam Aleikum!
Naomba kuelimishwa kuhusu yafuatayo:-

1) Mimi nimeolewa na mimba ya miezi mitatu ya bwana huyo huyo alienioa:-

a) Je, mtoto wangu halali au si halali?

b) Kwa kuwa mtoto huyo ni wa kike, inshallah akijaaliwa kuolewa, huyu baba anaweza kumuozesha?

c) Je, mtoto huyu anaweza kurithishwa mali ya baba huyu?


Huyu mume wangu tangu tuoane, huu ni mwaka wa 19 na bado naishi nae na tushazaa watoto wengine wa kiume wawili.

Nitashukuru kwa kujibiwa masuala yangu. Wabillahi Taufiq.

JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ahli zake, Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum jamiy'an) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukran kwa swali lako ambalo linahusiana na tatizo zito ovu lililoenea sana katika jamii yetu. Na ili sisi kuweza kuyaondoa ni lazima turudi vilivyo katika dini kwa kufuata Qur-aan Tukufu na Sunnah ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) la si hivyo basi tutakuwa na maisha ya dhiki hapa ulimwenguni na adhabu kali inatungoja kesho Akhera. Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ametuwekea kanuni za kuweza kuingiliana baina ya mume na mke, nje ya mahusiano hayo inakuwa ni haramu.
Jambo la kwanza ambalo tunafaa kuelewa ni kuwa mwanamke hawezi kuolewa akiwa ana mimba mpaka azae kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kumwaga mbegu za uzazi juu ya mbegu nyengine. Na ikiwa mwanamke ana mimba anaweza kuwa ameipata hiyo mimba ima kwa sababu alikuwa na mume au zinaa. Ikiwa alikuwa ana mume, na mume ameaga dunia au amemtaliki ni lazima azae, na huko kusubiri azae ndiyo eda yake.

a. Sasa kwa kuwa bwana huyo alikuoa ukiwa una mimba yake ambayo umeipata kabla ya ndoa, huyo mtoto utakayempata atakuwa ni wa zinaa. Na ilikuwa inatakiwa harusi au kukuoa ifanyike baada ya kuzaa kwako. Kuolewa huko na hali una mimba ni makosa.

b. Kishari’ah huyu mtoto anayezaliwa akiwa ni msichana au mvulana si wa baba na akiwa ni wa kike baba huyo wa kidamu hawezi kutoa idhini ya kumuozesha.

c. Baba na mtoto wa zinaa hawarithiani kabisa. Baba hamrithi mtoto wala mtoto hamrithi baba. Lakini mtoto anamrithi mama yake na mama anamrithi mtoto wake.

Jambo linalofaa nyinyi kufanya kwa sababu mumemkosea Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kuingia katika madhambi ni kurudi kwake na kumuomba msamaha, kuweka Niyah ya kutorudia tena kosa hilo na kufanya mema.
Na kadhalika ni kufunga ndoa upya kwa masharti yake kama yalivyo masharti ya ndoa.
Na tufahamu ya kwamba Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) ni Mwingi wa Kusamehe.
Na Allah Anajua zaidi.

    

SOMO JUU YA IMANI

IMANI INAPOMTAWALA MWANADAM, MAMBO YOTE YA KIDUNIA HUKOSA THAMANI'.....
 "Binti mmoja wa kiimerati kakubali kuolewa kwa mahari ya dirham moja (1) pekee, sawa na shillingi ishirin na mbili (22) za kenya, ama takriban mia nne (400)Tz. Jambo limewashangaza wazaz wa bwana harusi kwa uamuz wake binti kiasi alichoitisha, mfano mzuri wa kuiga kwa dada zetu kwa wale wenye iman ya kisawa" Mola awazidishie upendo na amani katika ndoa yao Na ABDULWAHAD at Turkey